MSANII wa muziki wa kizazi kipya Adili Mkwela anatarajia kutoa filamu mpya inayokwenda kwa jila la ‘Syndicate’. 

Akizungumza na mwandishi wetu alisema filamu hiyo itakuwa na vionjo vingi na kudai ataicheza kwa kutumia mazingira ya jiji la Mbeya.

Alisema filamu hiyo imeongozwa na Laurent Mwalugaja na kudai ipo chini ya kampuni ya Chapakazi.

“Ujio wa filamu ya Syndicate utakuwa wa aina yake kutokana na mazingira ambayo nimeyatumia.”Alisema Adili.